Skip to main content

Chuja:

dondakoo

UNICEF/Mahmood Fadhel

Watoto wengi walikosa chanjo muhimu mwaka 2018- Ripoti

Makadirio mapya yaliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na shirika la afya duniani WHO kuhusu masuala ya chanjo yanaonesha mwenendo wa hatari wa kuzorota kwa viwango vy utoaji chanjo kote duniani kutokana na vita, kutokuwepo kwa usawa na malalamiko.  Jason Nyakundi na maelezo zaidi.

Sauti
4'8"

15 Julai 2019

Miongoni mwa yale anayokuletea assumpta Massoi katika Jarida letu la Habari leo ni pamoja na 

-Kisa kipya cha Ebola chaibuka Goma DRC , shirika la afya WHO na serikali wanafanya kila njia kuzuia kusambaa kwa mlipuko huo

- Watoto milioni 20 hawakupata chanjo muhimu ya kuokoa maisha 2018 yasema mashirika ya UNICEF na WHO na kutaka kila nchi kuchukua hatua kuhakikisha watoto wote wanachanjwa

-Onyo limetolewa na shirika la afya duniani WHO kuwa vyakula vya watoto wachanga wa chini ya umri wa miezi sita vimejaa sukari

Sauti
12'15"

Dondakoo wasalia “mwiba” Yemen- WHO

Ugonjwa wa dondakoo unazidi kuwa tishio nchini Yemen baada ya kubainika kuwa hadi sasa hakuna chanjo dhidi ya ugonjwa huo kwa watoto wenye umri wa kuanzia miaka mitano na kuendelea pamoja na vijana.

Shirika la afya duniani WHO linasema ingawa dozi 100,000 za kutibu dondakoo ziliwasili Jumatatu, dawa hizo ni kwa watoto walio na chini ya umri wa miaka mitano.

WHO imetaka hatua zaidi za kufungua mipaka ili misaada ya kibinadamu pamoja na dawa ziwafikie walengwa haraka ikwezekanavyo.

WHO yahaha kukabili mlipuko wa dondakoo Yemen

Shirika la afya ulimwenguni, WHO limeanza kusambaza dawa ili kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa dondakoo nchini Yemen.

Mwakilishi wa WHO nchini Yemen Dkt, Nevio Zagaria amesema hatua hiyo ni muhimu ili kuondoa aibu itokanayo na watoto kufariki dunia kwa ugonjwa huo wenye chanjo.

Amesema tayari shehena ya dawa za kutibu ugonjwa huo imewasili baada ya njia za anga, majini na ardhini kufunguliwa kufuatia kufungwa kwa wiki tatu.