Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News

Afrika yapazia sauti mambo 6 COP25

Wakati mkutano huo wa COP25 ukiendelea mashirika ya asasi za kiraia kutoka barani Afrika yakiwakilisha nchi zaidi ya 40, chini ya mwamvuli wa Muungano wa Afrika wa haki na tabianchi (PACJA), yamedai jumuiya ya kimataifa kuchapuza mchakato na maamuzi yatakayozingatia mazingira na maslahi ya bara hilo .

Sauti
6'9"
UN News

Harakati za kupinga ukatili dhidi ya wanawake kwenye maeneo ya migodi Uganda zashika kasi

Siku 16 za kimataifa za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na wasichana zikiendelea kuangaziwa duniani, ni wazi kuwa ukatili wa kijinsia ni changamoto ya ulimwenggu ukiwa na madhara makubwa kwa watoto wa kike na wanawake.  Nchini  Uganda uzinduzi wa filamu itwayo ‘Wanawake Hushikilia Anga’ ni miongoni mwa harakati za asasi za kiraia zilizofanyika nchini humo katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia. Je nini kimefanyika, ungana basi na John Kibego katika, ambaye amekuwa shuhuda wetu.

Sauti
3'32"
UNDP Bhutan/NPIF

IFAD yawezesha Bhutan kuendelea kupata mlo wao wa asili mezani

Mkutano wa 25 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP25 unaanza leo  huko Madrid, Hispania kuangazia hatua zinazochukuliwa kuhakikisha kuwa hatua sahihi za kulinda tabianchi zinatekelezwa, wakati huu ambapo ni miaka 4 sasa tangu kupitishwa kwa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi. Hatua zinazopaswa kuchukuliwa ni pamoja na kupunguza hewa chafuzi na kuzingatia kilimo endelevu kisichoharibu mazingira sambamba na kilimo cha mazao ya asili.

Sauti
4'9"