Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala ya Wiki

Picha na UNCTAD/Adam Kane

Asasi ya kiraia yasaidia wanawake wanavikundi Geita Tanzania

Katika kufanikisha ustawi wa wanawake katika jamii, watu binafsi ikiwemo wanawake wenyewe wanajizatiti kujiimarisha kimaisha huku wakipata msaada kwa kuungana katika vikundi. Adelina Ukugani wa redio washirika Storm FM Geita amezungumza na wanawake wana vikundi ambao wanapata ushauri na usaidizi kutoka kwenye asasi ya kiraia ya Women’s Promotion Centre (WPC) huko Mgusu mkoani Geita nchini Tanzania.

Sauti
5'7"
FAO

Mabadiliko ya tabianchi yanaathiri mazao ya asili

Wakati wa maadhimisho  ya chakula duniani tarehe 16 mwezi huu wa Oktoba, suala la lishe bora liliangaziwa na zaidi ya yote nafasi ya vyakula asili. Hata hivyo mabadiliko ya tabianchi yameleta tafrashi katika baadhi ya maeneo ikiwemo Kagera nchini  Tanzania ambako mazao ya asili yametoweka. Je hali iko vipi? Ungana  basi na Nicolaus Ngaiza wa radio washirika Kasibante FM kwa ufafanuzi zaidi.

 

Sauti
8'31"
UN News/Grece Kaneiya

Elimu ni sehemu ya maendeleo na bila mwalimu hakuna elimu-Mwalimu Tabichi

Leo katika mada kwa kina tunaangazia siku ya walimu duniani ambayo huadhimishwa Oktoba 5 kila mwaka, mwaka huu kaulimbiu ikiwa ni “walimu vijana, mustakbali wa tasnia hii.” Lengo la siku ya walimu ikiwa ni kuwaenzi walimu kote ulimwenguni, kupongeza mafanikio na kuangalia changamoto zilizopo  kwa ajili ya kuimarisha tasnia hiyo. Mgeni wa siku ya leo kwa sasa anashikilia tuzo ya mwalimu bora kimataifa, tuzo ambayo ametunukiwa mapema mwaka huu kufuatia kujitolea kwake katika kazi ualimu.

Sauti
5'57"