Asasi ya kiraia yasaidia wanawake wanavikundi Geita Tanzania
Katika kufanikisha ustawi wa wanawake katika jamii, watu binafsi ikiwemo wanawake wenyewe wanajizatiti kujiimarisha kimaisha huku wakipata msaada kwa kuungana katika vikundi. Adelina Ukugani wa redio washirika Storm FM Geita amezungumza na wanawake wana vikundi ambao wanapata ushauri na usaidizi kutoka kwenye asasi ya kiraia ya Women’s Promotion Centre (WPC) huko Mgusu mkoani Geita nchini Tanzania.