Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Redio yatumia lugha asilia kusaidia umma nchini Kenya

Nchini Kenya redio kama ilivyo katika nchi nyingine hutumika kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu wakati wa majanga na kwa kupitia lugha za asili ujumbe umekuwa ukiwafikia walengwa kwa namna rahisi.

Ungana na Geoffrey Onditi wa redio washirika KBC katika makala inayofafanua namna redio inavyotumia fursa ya lugha hizo akusaidia wakati wa majanga.

Radio imetumika sana kupasha habari hususan wakati wa majanga- Mbotela

Umuhimu wa Radio bado ni dhahiri katika mataifa yanaoendelea na hususan wakati wa dharura. Katika ujumbe wa mwaka huu katika kuadhimisha siku ya Radio Duniani ambayo ni Februari 13, Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limesema kwamba radio ina mchango mkubwa wakati wa kukabiliana na majanga.

Katika mahojiano yafuatayo kutoka Kenya Geoffrey Onditi wa radio mojawapo ya washirika wetu, KBC, amezungumza na mtangazaji gwiji Leonard Mambo Mbotela, mwenye umaarufu unaovuka mipaka ya Kenya, akimweleza umuhimu wa chombo hiki adhimu.

UNAMID redio na wajibu wake katika mizozo Sudan

Siku ya radio duniani hudhimishwa tarehe 13 Februari kila mwaka, mwaka huu inaaadhimishwa sambamba na miaka 70 ya redio ya Umoja wa Mataifa huku umuhimu wa redio katika majanga ikiwa ni maudhui mwaka huu. Nchini Sudan hususani katika jimbo la Darfur redio ya ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika jimboni humo UNAMID pamoja na mambo mengine inatekeleza wajibu muhimu wa kuzipatia fursa za kushiriki kwenye majadiliano pande kinzani ili kupata amani ya kudumu.

Jinamizi la kukeketwa linanitesa:Keziah

"Nikiona nyembe au vitu vyenye ncha kali nakumbuka nilivyokeketwa”Ni kauli ya manusura wa mila potofu ya ukeketaji kutoka Kenya Keziah Oseko ambaye amekutana na mwandishi wa idhaa hii Joseph Msami kandoni mwa mkutano kuhusu kupinga kitendo hicho.

Mwanaharakati huyo kadhalika amesema kuwa ni wajibu wa jamii kukemea kitendo hicho ili kufanikisha kampeni dhidi ya ukeketaji. Kwanza anaanza kulezea lini hasa alianza harakati hizo.

Mtandao wa kuendeleza uhifadhi wa mazingira vyuoni wazinduliwa Kenya

Mtandao mpya umezinduliwa leo na Shirika la Mpango wa Mazingira, UNEP, ukilenga kujumuisha vitendo vya kutunza mazingira na kukuza uendelevu katika mitaala na miradi ya utafiti ya vyuo vikuu nchini Kenya.

Zaidi ya washiriki 160 wamehudhuria hafla ya kuzinduliwa kwa mtandao huo wa Kenya Green Universities Network jijini Nairobi, ambao ni mkakati wa pamoja wa Kamisheni ya Elimu ya Vyuo Vikuu nchini Kenya (CUE), Mamlaka ya Udhibiti wa Mazingira (NEMA), na Shirika la Mpango wa Mazingira (UNEP).

Fistula bado tatizo, UNFPA Tanzania wapania kuitokomeza

Fistula! Ugonjwa unaowakumba wanawake na wasichana kutokana na kuchelewa kupata huduma stahiki wakati wa kujifungua. Takwimu zinaonyesha kuwa licha ya mafanikio katika mbinu za kisasa za kutoa huduma ya afya bado takriban wanawake 800 wanafariki dunia kutokana na maradhi yatokanayo na uja uzito kila siku na kwa kila mwanamke anayefariki takriban wanawake 20 wanapata majeraha ya maisha kama vile fistula.

Wadau wote wanapaswa kushiriki vita dhidi ya ukeketaji:UNFPA

Nchi mbalimbali zimekuwa zikichukua hatua ikiwa ni pamoja na kuelimisha umma, na wadau wote wakiwemo mangariba.

Kampeni kubwa inafanywa na shirika la Umoja wa mataifa la idadi ya watu UNFPA inayosistiza kwamba wadau wote katika jamii ikiwemo serikali , viongozi wa dini na mangariba wanapaswa kushiriki vita hivi.

Florence Gachanja ni afisa mipango wa UNFPA Kenya amezungumza na Flora Nducha wa idhaa hii na anaanza kwa kufafanua hali ya tatizo hili nchini Kenya.

(MAHOJIANO NA  FLORENCE)

Vijana wajiongeze ili kushika fursa za kiuchumi na kisiasa: Francine Muyumba #Youth2030

Barani Afrika, vitisho vya kigaidi kutoka vikundi vya waasi kama vile Boko Haram nchini Nigeria au ADF-Nalu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC vimesababishwa na vijana wa maeneo hayo kukataa tamaa na kukosa fursa za kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Hayo ni maoni ya Francine Furaha Muyumba ambaye ameshiriki Kongamano la vijana lililofanyika wiki hii mjini New York, Marekani na kujumuisha wawakilishi zaidi ya 800 na mawaziri 21 kutoka nchi mbali mbali wanachama wa Umoja wa Mataifa.

Vita dhidi ya vikundi vya misimamo mikali ni lazima vianzie mashinani:Dkt. Ali

Februari mosi hadi saba ni wiki ya kuadhimisha  uwiano baina ya imani mbalimbali za kidini ulimwenguni. Wiki hii ilitengwa na Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kupitia azimio la tarehe 20 Oktoba mwaka 2010. Azimio hilo pamoja na mambo mengine linataja uelewa na mazungumzo baina ya dini mbalimbali kama kiungo muhimu katika kuimarisha maelewano miongoni mwa watu wengi licha ya Imani zao.