Maadhimisho ya muongo wa watu wenye asili ya afrika
Kwa zaidi ya miaka mia 400, biashara ya utumwa imekuwa janga lililoikumba Afrika, ikikadiriwa kwamba zaidi ya watu milioni 15, wanaume, watoto na wanawake wamekuwa wahanga wa biashara hii kupitia bahari ya Atlantiki.
Hadi leo, Umoja wa Mataifa unakadiria kwamba watu wapatao milioni 200 wenye asili ya Afrika wanaishi Marekani na kwenye bara la Amerika na Karibia.
Wengi wao bado hukumbwa na unyanyapaa na ubaguzi, wakikosa fursa sawa za kielimu, kisiasa na kiuchumi.