uhifadhi wa sauti na video Afrika Mashariki
Oktoba 27 ni siku ya kimataifa ya uhifadhi wa sauti na video.Siku hii ambayo ilipitishwa mwaka 2005 na BAraza Kuu la Umoja wa Mataifa inalenga kuchagiza uelewa wa hatua madhubuti za utunzaji wa nyaraka za sauti na video kama kiungo muhimu cha utambulisho wa kitaifa.
Katika ujumbe wa mwaka huu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni UNESCO, Irina Bokova amesema kwamba kuna miaka 10 hadi 15 ya kubadilisha sauti za video zilizopo kutoka analojia kwenda dijitali ili kuhakikisha uhifadhi wake.