Sekta ya huduma kuinua Afrika, UNCTAD yafungua ofisi Addis Ababa
Tarehe Tisa Julai mwaka huu, Shirika la biashara na maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNCTAD lilizindua ripoti kuhusu uchumi barani Afrika! Jambo kubwa katika ripoti hiyo ni umuhimu wa sekta ya huduma katika kukwamua uchumi wa bara hilo ambalo kwa miongo zaidi ya mitano imekuwa ikipatia kipaumbele sekta ya viwanda na kilimo.