Shamrashamra za miaka 55 ya Uhuru wa Somalia
Pakua
Somalia, nchi ambayo imekuwa katika vita kwa zaidi ya miongo miwili sasa inaibuka kutoka katika majivu ya vita hivyo vya wenyewe kwa wenyewe. Changamoto bado zipo, iwe kisiasa, kiuchumi na kijamii lakini changamoto hizo hazikuzuia serikali ya shirikisho na wananchi kusherehekea miaka 55 ya uhuru wa nchi hiyo. Sherehe zilifanyika maeneo mbali mbali ikiwemo Baidoa, Beletweyne na Kismayo. Lakini katika makala hii, Assumpta Massoi anakupeleka Mogadishu, mji mkuu wa Somalia ambako ndiko sherehe za kitaifa zilifanyika na kuhudhuriwa na wananchi na wageni mbali mbali.