Umuhimu wa familia katika jamii nchini Kenya
Siku ya familia duniani imekuewa ikiadhimishwa Mei 15 kila mwaka tangu ipitishwe na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 1993. Lengo ni kutoa fursa ya kuchagiza uelewa kuhusu taasisi hiyo muhimu kabisa ili kuimarisha maarifa kuhusu maswala ya kijamii, kiuchumi na mabadiliko yanayoathiri familia.
Kauli mbiu ya mwaka huu ya je wanaume wanawajibika? Inalenga kuimarisha usawa wa kijinsia na haki za watoto katika familia. Aidha unapigia chepuo kuzuia ukatili katika familia kupitia sheria na mikakati na programu za kuingilia kati.