Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

02 Machi 2021

Hii leo jaridani, Flora Nducha anaanzia huko Somaliland ambako Umoja wa Mataifa umepeleka mashine za kuwezesha wagonjwa kuvuta hewa ya oksijeni wakati huu hospitali zimezidiwa kutokana na  janga la COVID-19 linaloleta mkwamo kwa wagonjwa kupumua. Kisha anammulika Mkurugenzi Mkuu mpya wa shirika la biashara duniani, WTO, Ngozi Okonjo-Iweala ambaye amenaza rasmi jukumu lake akiwa mwanamke wa kwanza na pia mwafrika wa kwanza kushika wadhifa huo.

Sauti
14'3"

01 Machi 2021

Hii leo jumatatu ya Machi Mosi ni mada kwa kina tukimulika mshindi wa tuzo ya Umoja wa Mataifa huko nchini kenya ambaye anatumia taka za plastiki kutengeneza matofali ya kutengenezea barabara Lakini kuna muhtasari wa habari ukimulika ubaguzi duniani, mwandishi wa habari kufariki dunia baada ya kuswekwa rumande huko Bangladesh na shambulizi huko Yemen. Mashinani tunaangazia COVID-19 na UKIMWI. Karibu na mwenyeji wako ni Flora Nducha.