Wawanufaisha Wanawake na watoto Malawi wanufaika na mradi wa kukuza lishe (SUN)
Mradi wa ushirikiano kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na Seriali ya Malawi kuboresha hali ya lishe ya wanawake wajawazito, akina mama na watoto wenye umri chini ya miaka mitano umekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi nchini Malawi. Taarifa inasomwa na Hilda Phoya.
Mradi wa kuboresha hali ya lishe ili kupambana na utapiamlo katika wilaya sita za nchini Malawi, ni msaada mkubwa wa kidunia ambao unazileta pamoja nchi kadhaa katika juhudi za kuweka sera za nchi katika kutekeleza mipango yenye malengo ya pamoja kuhusu lishe.