Ubunifu wa nguo za magome ya miti na uhifadhi wa mazingira Burundi-Sehemu ya II
Katika Juhudi za kuunda ajira na kuhifadhi mazingira, msichana kutoka Burundi Annick Kabatesi ameanzisha mradi wa kutengeneza nguo zitokanazo na magome ya miti. Nguo hizo zimetajwa kuwa zinazingatia uhifadhi wa mazingira. Bi. Kabatesi ambaye ni mwanamitindo pia amejijengea umaarufu mkubwa kwa kutengeneza nguo hizo za magome ya miti baada ya nguo hizo kuwavutia viongozi wakuu Serikalini.