Guterres asikitishwa na shambulio la New York
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameelezea kusikitishwa na kutiwa hofu na shambulio llilofanyika jijini New York Marekani Jumanne, katika mji ambao ndiko makao makuu ya Umoja wa Mataifa.
Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Bwana Guterres ametuma salamu zake za rambi rambi kwa familia za wahanga na kuwatakia afueni ya haraka majeruhi.