FAO yaleta unafuu kwa wanawake wanaofuga kuku Gambia
Shirika la chakula na kilimo duniani, FAO limesema miradi yake katika nchi za Afrika imeanza kukwamua wanawake wajasiriamali kwa kuwawezesha kuinua vipato na wakati huo huo kuhakikisha upatikanaji wa chakula.
Afisa mwandamizi FAO anayehusika na usawa wa kijinsia na maendeleo vijijini Thacko Ndiaye amesema hayo katika mahojiano na Idhaa ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambako anahudhuria mkutano wa 61 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW61.