Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Tunahitaji fedha za dharura kusaidia wakimbizi wa Iraq: UNHCR

Idadi ya wanaofurushwa makwao ikiongezeka Magharibi mwa Mosul nchini Iraq, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linafungua kambi mpya sambamba na wito wa usaidizi kwa wafadhili kuongeza fedha kwa ajili ya ulinzi na malazi kwa wanaofurushwa.

Kwa mujibu wa taarifa ya UNHCR, watu 255,000 wamefurushwa kutoka Mosul na maeneo ya karibu tangu mwezi Oktoba mwaka jana, ikiwa ni pamoja na zaidi ya 100,000 tangu kampeni ya kijeshi iliponza Magharibi mwa mji huo mnamo Januari 19.

Hakuna pengo la mishahara baina ya wanawake na wanaume Tanzania: Kigwangalla

Serikali ya Tanzania imesema injivunia hatua zilizopigwa katika suala la ukombozi wa mwanamke katika nyanja mbalimbali ikiwemo kisheria, kiuchumi, kisiasa na hata kijamii.

Kauli hiyo imetolewa na naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto, Dr Hamisi Kigwangalla alipohojiwa na idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kandoni mwa kikao cha 61 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani kinachoendelea kwenye Umoja wa Mataifa.

Akigusia moja ya changamoto kubwa za kimataifa kuhusu pengo la asilimia 23 katika mishahara baina ya wanaume na wanawake amesema

Usugu wa viuavijasumu ni tisho kwa kwa maendeleo endelevu: UM

Usugu wa viuavijasumu au antimicrobial resistance AMR ni tisho kubwa la kutimiza ajenda ya 2030 ya maendeleo endelevu amesema naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed.

Amesema hayo hivi leo Alhamisi kwenye makau makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York walipokuwa wakijadili swala hilo na mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO Dkt. Margaret Chan.

Bi Mohamed amesema dhamira ya kuundwa kwa kundi maalum la kushughulia na tatizo ni hilo kwa ngazi za juu ni kupambana AMR, na kushauriana kuhusu jitihada za kimataifa jinsi wanavyokabiliana na tisho hilo.

Mkurugenzi Mkuu wa IOM alaani shambulio dhidi ya msafara wa wahudumu wa kibinadamu Sudan Kusini

Mkurugeni mkuu wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM William Lacy Swing,  hivi leo amelaani shambulizi dhidi ya msafara wa wafanyi kazi wa misaada ya kibinadamu nchini Sudan Kusini liotokea Machi 14 na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine watatu kujeruhiwa. Wafanyi kazi hao walivamiwa na watu wenye silaha wasiojulikana walipokuwa  wanarudi Yirol Mashariki mwa Sudan Kusini baada ya operesheni za kibinadamu za kuokoa maisha kutokana na mlipuko wa kipindu pindu katika eneo hilo.

Ukatili na manyanyaso kazini ni ukiukaji wa haki za binadamu: ILO

Ukatili na manyanyaso kazini dhidi ya wanawake ni tatizo kubwa na la kimataifa limesema shirika la kazi duniani ILO.

Akizungumza kwenye mjadala maalumu kandoni mwa kikao cha 61 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani uliojadidili ukomeshaji wa ukatili wa wanawake kazini, , Manuela Tomei ambaye ni mkurugenzi wa idara ya hali ya kazi na usawa kwenye shirika la ILO amesema vitendo hivyo ni ukiukwaji wa haki za binadamu na vinaathiri utendaji wa kazi sio tu kwa waathirika, bali kwa viongozi na kampuni au mashirika wanayofanyia kazi , kwa hiyo ni lazima vikomeshwe

Zaidi ya raia 120,000 wamekimbia madhila magharibi mwa Mosul, Iraq

Tangu vikosi vya kijeshi nchini vianze mapigano ya kukomboa mji wa Mosul mwezi Oktoba mwaka, takribani raia 345,000 wamekimbia makwao, ambapo 275,000 kati yao wanahitaji usaidizi.

Amesema mratibu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq Bi Lise Grande akizungumza na waandishi wa habari hii leo kwa njia ya video kutoka Iraq.

Ameongeza inakadiriwa kuna raia zaidi ya Laki Nane magharibi mwa Mosul ambako mapigano ya kukomboa yalianza mwezi Februari na tayari zaidi ya 120,000 wamekimbia makazi yao..

(Sauti ya Lise Grande)

Shilingi 5,000 zimebadili maisha yangu: Mjasiriamali

Mjasiriamali kutoka Tanzania Bi Amina Shaaban anasema amefanikiwa kusomesha watoto wake kwa kuanzia na mtaji wa shilingi 5,000 za Tanzania ambapo aliitumia kuuza nazi nakupata faida.

Bi Amina ni miongoni mwa wanawake wa Tanzania Zanzibar, hususani Pemba, ambao wamenufaika baada ya serikali kuelimisha wanawake namna ya kujikomboa kiuchumi ili kukabiliana na chnagamoto ya ajira.

Ungana na Khadija Kombo wa redio washirika Micheweni redio ya Pemba katika makala itakayokupa undani wa taarifa hii ya kusisimua.

Tunawasaka waliotekwa nyara DRC-Dujarric

Umoja wa Mataifa umesema unaendelea na msako dhidi ya wataalamu wa kimataifa wawili na wafanyakazi watatu raia wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC ambao walitekwa nyara na watu wasiojulikana jimboni Kasai nchini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani msemaji wa Katibu Mkuu wa umoja huo Stéphane Dujarric amesema malalamiko ya serikali ya DRC kuhusu kutoarifiwa kuhusu uwepo wa wafanyakazi hao yatajibiwa na maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini humo na kuongeza kuwa kwa sasa mwelekeo ni kuendelea kuwasaka watu hao walioko kusikojulikana.

Guterres azungumzia mapendekezo ya bajeti ya Marekani 2018

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema ameazimia kufanyia marekebisho chombo hicho na kuhakikisha kuwa kinakidhi malengo na kuleta matokeo bora kwa gharama yenye unafuu.

Bwana Guterres amesema hayo kufuatia Ikulu ya Marekani kuweka wazi mapendekezo ya bajeti ya nchi hiyo kwa mwaka wa 2018, mapendekezo ambayo inaelezwa yanalenga kupunguza matumizi kwenye maeneo kadhaa ikiwemo ushirikiano wa kimataifa na kuongeza pesa kwenye matumizi ya kijeshi.