Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Zaidi ya watu milioni 7 wanakumbwa na baa la njaa bonde la ziwa Chad:UM

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo liko nchini Chad ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya nchi nne kuangazia changamoto zinaoendelea za kibinadamu katika eneo la bonde la ziwa Chad  na kuongeza uelewa wa kimataifa kwa hatma ya watu wapatao milioni 11.

Ujumbe wa baraza hilo ukiwa katika mji mkuu N'Djamena umekutana na waziri mkuu Albert Pahimi Padacké na pia kutembelea kikosi cha pamoja cha askari kutoka nchi nne zilizoathirika kwenye kanda hiyo ikiwemo Cameroon, Chad, Niger na Nigeria, pamoja Benin wanakokabiliana na mapambano dhidi ya Boko Haram.

Kuepusha zahma Sudan Kusini msaada lazima ufike sasa: O'Brien

Mamia kwa maelfu ya watu nchini Sudan Kusini wataathirika zaidi na baa la njaa endapo wafanyakazi wa misaada hawatapata fursa ya kuwafikishia msaada waathirika na fedha zaidi za ufadhili kutolewa ameonya hii leo mratibu wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa Stephen O'Brien.

Amesema hayo baada ya kusafiri hadi eneo la Ganyiel, jimbo la Unity,  moja ya maeneo yenye vurugu na kukutana na watoto walio kwenye hali mbaya ya utapiamlo.

Uhai wa wanyamapori ni uhai wetu- UNEP

Tarehe tatu mwezi Machi ya kila mwaka ni siku ya wanayamapori duniani. Kauli mbiu ya mwaka huu ni kusikiliza sauti za vijana ambao wana fursa ya kuhakikisha urithi wa wanyamapori kwa vizazi vijavyo.

Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP, kuwaenzi wanyamapori na maliasili ambalo ni jumuku la serikali na sekta binafsi na hata raia linahitaji hatua madhubuti na hivyo katika ujumbe kupitia tovuti hususani Twitter, shirika hilo limehamasisha dunia kulinda viumbe hai na maliasili kwa kusema “ Fanya jambo moja leo”

Watu wanaotawanywa na machafuko kwa siku Mosul ni 4,000

Idadi ya watu wanaotawanywa kwa siku Mosoul Iraq kutokana na operesheni za kijeshi zinazoendelea dhidi ya kundi la kigaidi la ISIL na hofu ya matumizi ya silaha za ckemikali dhidi ya raia imeongezeka sana.

Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR sasa watu 4000 kwa siku wanakimbia kutoka Magharibi mwa Mosoul sehemu ambayo kwa kiasi kikubwa inadhibitiwa na waasi wenye itikati kali.

UN Photo/Evan Schneider

Muenzini Maathai kwa kuhifadhi mazingira : UNEP

Leo ni siku ya mazingira barani Afrika, siku ambayo pia imepewa heshima ya kuitwa siku ya Wangari Maathai,mwanaharakati wa mazingira kutoka Kenya ambaye enzi za uhai wake alipigia chepuo uhifadhi wa mazingira.

Kupitia wavuti wake hii leo, Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP, limezitaka nchi za Afrika kuainisha mafaniko katika uhifadhi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya kumumezi mwanaharakati huyo.

Wanawake wa jamii za asili Australia wakabiliwa na ukatili mkubwa:UM

Mifumo mkingi ya ubaguzi imechochea kiwango kikubwa cha ukatili unaowakabili wanawake kutoka jamii za watu wa asili nchini austarlia. Hayo ni kwa mujibu wa mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu ukatili dhidi ya wanawake Dubravka Šimonović .

Bi Šimonović ambaye amekamilisha ziara nchini humo amesema wanawake wengi wanabaguliwa kimaumbile na kukabiliwa na ubaguzi wa rangi , lakini pia wanakumbwa na ubaguzi mwingine wa wa kuwekwa daraja la chini katika jamii kwa sababu ya hali yao ndogo kiuchumi.

Kismaayo yapata kituo cha kujenga stadi za vijana

Hii leo huko Kismaayo ambao ni mji mkuu wa muda wa jimbo la Jubaland nchini Somalia, kimefunguliwa rasmi kituo cha kusaidia kuwajumuisha kwenye jamii, DDR, wapiganaji wa zamani wa kikundi cha kigaidi cha Al –Shabaab.

Kituo hicho ni cha nne kufunguliwa nchini humo kama sehemu ya mpango wa kitaifa wa kuwapatia tiba na kuwalea wapiganaji hao wa zamani.

Ujenzi wake unatokana na ushirikiano kati ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, UNSOM, serikali ya Ujerumani, serikali kuu ya Somalia, serikali ya jimbo la Jubaland na wadau wa maendeleo.

Ukame ni janga la kitaifa Somalia: Rais Farmaajo

Rais mpya wa Somalia, Mohamed Abdullahi Farmaajo ambaye aliapishwa hivi karibuni ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kusaidia taifa lake kukabiliana na ukame ulioathiri zaidi ya raia milioni sita.

Akizungumza mjini Mogadishu kwenye mkutano wa ngazi ya juu kwa ajili ya ukame ambao amesema ni janga la kitaifa, Rais Farmaajo ameomba jumuiya hiyo kuongeza mchango wao wa dola million 825 ili kuzuia janga linaloweza kutokana na baa la njaa.

(Sauti ya Farmaajo)

UN Photo/Martine Perret

ITC kuinua wanawake kiuchumi Rwanda

Kituo cha kimataifa cha biashara ITC ambayo ni taasisi tanzu ya kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa UNCTAD na wadau, hii leo wametangaza ushirikiano mpya ili kusaidia wauzaji wa kahawa nje ya nchi, wasindikaji, na wakulima wa zao la buni nchini Rwanda.

Ushirikiano huo unalenga uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ambapo uboreshaji uwezo wa wa usindikaji wa kahawa nje ya nchi , kuongeza ubora wa zao hilo, kuongezeka kwa bei na kupunguza uchafuzi wa mazingira na matumizi mema ya maji vitazingatiwa.