Licha ya makataba wa amani , machafuko yafurusha maelfu Colombia-UNHCR
Licha ya kusainiwa kwa mkataba wa amani baina ya serikali ya Colombia na kundi la upinzani liitwalo FARC, mwezi Novemba mwaka jana, machafuko nchini humo yanaendelea kufurusha maelfu ya watu, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.
Mapigano baina ya vikosi hivyo yamedumu kwa miaka 50.
UNHCR licha ya kutambua juhudi za kusaka amani na kuhakikisha haki za wahanga, shirika hilo limeeleza kusikitishwa na kuongezeka kwa kiwango cha wakimbizi.