India na Ufaransa kuunda setilaiti ya kuchambua tabianchi
India na Ufaransa zitaingia makubaliano ya kuunda setilaiti inayochambua mabadiliko ya tabianchi.
Hatua hiyo inafuatia mazungumzo kati ya Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na Rais Francois Hollande wa Ufaransa ambapo taasisi mbili za masuala ya anga za juu za nchi hizo zitahusika na utengenezaji.
Mpango huu unaimarisha ushirikiano wa awali kati ya taasisi hizo za ISRO ya India na CNES ya Ufaransa ambapo tayari walishatengeneza setilaiti mbili za kutoa takwimu za uchambuzi wa tabianchi. Setilaiti hizo zinafuatilia vyanzo vya maji na uhakika wa chakula.