Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mratibu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Lebanon Sigrid Kaag azuru Iran

Mratibu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Lebanon Sigrid Kaag azuru Iran

Pakua

Mratibu Maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Lebanon Bi. Sigrid Kaag, Jumapili amekutana na maafisa wa serikali ya Iran mjini Tehran.

Mratibu huyo maalumu amejadili na maafisa wa serikali kuhusu hali ya kisiasa nchini Lebanon, maendeleo ya kikanda yanayoathiri Lebanon na juhudi za kuchagiza utulivu na usalama katika kanda nzima.

Wakati za ziara hiyo Bi Kaag pia amekutana na wawakilishi wa jumuiya ya kidiplomasia. Ziara yake nchini Iran imefanyika kama sehemu ya majadiliano yanayoendelea na mratibu huyo maalumu na wadau wengine muhimu katika kanda.