Kiongozi wa OCHA aangazia hali ya kibinadamu Eritrea na Ethiopia
Naibu Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu, OCHA, Kyung-wha Kang, amehitimisha ziara ya siku tatu nchini Eritrea akisihi jumuiya ya kimataifa kuongeza usaidizi wake kwa watu wanaoishi kwenye mazingira magumu nchini humo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Bi Kang amekutana na viongozi wa serikali na kutembelea vituo vya afya vinavyoongozwa na serikali kwenye baadhi ya maeneo ya nchi, akishuhudia hatua zilizopigwa na serikali katika kuimarisha afya ya mama na mtoto.