UM wathibitisha vikosi vya Kenya kuingia Somalia
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augstine Mahiga leo amethibitisha kwamba vikosi vya jeshi la Kenya vimeingia Somalia.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augstine Mahiga leo amethibitisha kwamba vikosi vya jeshi la Kenya vimeingia Somalia.
Serikali ya Tanzania imeitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza juhudi na kunyoosha mkono zaidi kusaidia kunusuru maisha ya mamilioni ya watu nchini Somalia.
Nchi nyingi zinazoendelea bado hazijamudu kukabiliana na athari za majanga ya asili na hata yanayosababishwa na shughuli za binadamu. Hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha siku ya kimataifa hii leo ya kupunguza majanga.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasaidia maelfu ya raia wa Sudan Kusini kurejea nyumbani.
Kwa mujibu wa shirika hilo maelfu ya raia hao wengi walikuwa wamekwama katika eneo la Kosti na wengine ni wale walioishi Kaskazini kwa muda na sasa wanataka kurudi nyumbani.
Kikao cha 20 cha kimataifa cha kundi la Somalia, kimekamilisha mkutano wa siku mbili mjini Copenhagen, nchini Denmark. Mkutano huu umezungumzia mipango wa kumaliza kipindi cha mpito cha serikali ya mpito ya Somalia ifikapo Agosti 12.
Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga amesema kifo cha mwanamazingira wa Kimataifa na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Profesa Wangari Maathai ni pigo kubwa kwa Kenya.
Serikali ya Kenya imesema licha ya changamoto za fedha, vifaa na wataalamu imejiandaa na kuweka mikakati ya kitaifa kukabiliana na maradhi yasiyo ya kuambukiza.
Watu wasiopungua 40 wameuwawa nchini Burundi katika shambulio la watu wenye silaha kwenye wilaya ya Gatumba nje kidogo ya mji mkuu wa nchi hiyo Bujumbura . Serikali ya Burundi imetangaza msiba wa kitaifa na maombolezo kwa siku tatu.
Wiki hii dunia imeadhimisha siku ya kimataifa ya kujua kusoma na kuandika, takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa watu zaidi ya milioni 700 duniani na hasa watu wazima hawajui kusoma na kuandika.