Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Rais Nkurunziza akatisha safari kwenye UM baada ya mauaji nchini Burundi

Rais Nkurunziza akatisha safari kwenye UM baada ya mauaji nchini Burundi

Pakua

Watu wasiopungua 40 wameuwawa nchini Burundi katika shambulio la watu wenye silaha kwenye wilaya ya Gatumba nje kidogo ya mji mkuu wa nchi hiyo Bujumbura . Serikali ya Burundi imetangaza msiba wa kitaifa na maombolezo kwa siku tatu.

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ambaye angeianza ziara hii leo kuelekea nchini Marekani kuhudhuria kikao cha Baraza kuu la Umoja wa Mataifa ambalo limeanza kujadili maradhi yasiyo ya kuambukiza ameahirisha safari yake.

Mwandishi wetu wa Burundi Ramadhan Kibuga na taarifa kamili.

(RIPOTI YA RAMADHAN KIBUGA)