Nchi zinazoendelea zinahitaji msaada kukabiliana na majanga
Nchi nyingi zinazoendelea bado hazijamudu kukabiliana na athari za majanga ya asili na hata yanayosababishwa na shughuli za binadamu. Hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha siku ya kimataifa hii leo ya kupunguza majanga.
IOM yasaidia kuwarejesha nyumbani raia wa Sudan Kusini
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasaidia maelfu ya raia wa Sudan Kusini kurejea nyumbani.
Kwa mujibu wa shirika hilo maelfu ya raia hao wengi walikuwa wamekwama katika eneo la Kosti na wengine ni wale walioishi Kaskazini kwa muda na sasa wanataka kurudi nyumbani.
Kikao kuhusu Somalia chakamilika mjini Copenhagen
Kikao cha 20 cha kimataifa cha kundi la Somalia, kimekamilisha mkutano wa siku mbili mjini Copenhagen, nchini Denmark. Mkutano huu umezungumzia mipango wa kumaliza kipindi cha mpito cha serikali ya mpito ya Somalia ifikapo Agosti 12.
Kifo cha Wangari Maathai ni pigo kubwa kwa Kenya:Odinga
Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga amesema kifo cha mwanamazingira wa Kimataifa na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Profesa Wangari Maathai ni pigo kubwa kwa Kenya.
Kenya imeandaa mikakati kukabili NCD's:Mugo
Serikali ya Kenya imesema licha ya changamoto za fedha, vifaa na wataalamu imejiandaa na kuweka mikakati ya kitaifa kukabiliana na maradhi yasiyo ya kuambukiza.
Rais Nkurunziza akatisha safari kwenye UM baada ya mauaji nchini Burundi
Watu wasiopungua 40 wameuwawa nchini Burundi katika shambulio la watu wenye silaha kwenye wilaya ya Gatumba nje kidogo ya mji mkuu wa nchi hiyo Bujumbura . Serikali ya Burundi imetangaza msiba wa kitaifa na maombolezo kwa siku tatu.
Bila kujua kusoma na kuandika hakuna maendeleo:UM
Wiki hii dunia imeadhimisha siku ya kimataifa ya kujua kusoma na kuandika, takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa watu zaidi ya milioni 700 duniani na hasa watu wazima hawajui kusoma na kuandika.
Bila kujua kusoma na kuandika kuendelea ni vigumu:M
Wakati dunia ikiadhimisha siku ya kimataifa ya kufuta ujinga kwa kujua kusoma na kuandika, Umoja wa Mataifa unasema bila kutatua tatizo hilo linalowakabili watu zaidi ya milioni saba duniani amani na maendeleo itaendelea kuwa ndogo.
Mkutano wa kuomba msaada kwa ajili ya pembe ya Afrika kufanyika Addis Ababa
Mkutano wa Kimataifa ulioandaliwa na Umoja wa Afrika kwa ajili ya kuomba msaada wa kukabiliana na matatizo yanayoikabili pembe ya Afrika hivi sasa utafanyika kesho Alhamisi mjini Addis Ababa Ethiopia.