Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama la UM limelaani vikali shambulio dhidi ya MINUSMA

Mkutano wa Baraza la Usalama kujadili mauaji wa walinda amani wa MINUSMA nchini Mali. Picha: UM

Baraza la Usalama la UM limelaani vikali shambulio dhidi ya MINUSMA

Wajumbe wa Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa wamelaani vikali mashambulizi dhidi ya vikosi vya walinda amani vya ujumbe wake Mali   (MINUSMA) katika eneo la Ménaka, lililofanyika Novemba 24, 2017, na kusababisha vifo vya askari 3  kutoka Nigeria, na kujeruhiwa wengine 21.

Wajumbe  wa baraza la usalama wametuma salamu zao za rambirambi kwa familia za wafiwa, serikali ya Nigeria na pia ujumbe wa  MINUSMA  huku   wakiitaka mamlaka ya Mali kuchukua hatua za kisheria ili kuhakikisha  wahusika wanatiwa nguvuni na vyombo vya dola.

Aidha wajumbe wasema  kamwe hawatafumbia macho vita dhidi ya ugaidi kwa njia zozote na kuahahakikisha unakomeshwa kabisa na pia wamezitaka  serikali zote duniani kushirikiana  katika vita dhidi ya mitandao yote ya kigaidi kwa nguvu zote.

Pia wamesema ni lazima kuiwezesha MINUSMA katika  kuhahakisha wanapata vitendea kazi kwa mujibu wa Azimio la Baraza la Usalama 2364 (2017) ili kuweza kujilinda na pia kulinda maeneo wanayoyahudumia  huko  Mali na sehemi nyingne.