Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tunafuatilia kwa karibu kinachoendelea Tunisia:UN

Picha: OHCHR

Tunafuatilia kwa karibu kinachoendelea Tunisia:UN

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa leo imesema kuwa inafuatailia  kwa karibu maanadamano yanayoendelea nchini Tunisia , athari zake na hatua zinazochukuliwa  na serikali ya nchi hiyo. Siraj Kalyango ana maelezo zaidi.

(TAARIFA YA SIRAJI KALYANGO)

Kwa mujibu wa msemaji wa ofisi ya hiyo,Rupert Colville, hofu yao ni kuhusu idadi kubwa ya watu wanaokamatwa katika maandamano hayo yamepelekea watu 778 kukamatwa tangu jumatatu,kati ya hao 200 ni wale wenye umri ulio kati ya 18 na 21.

Msemaji huyo ametoa mwito kwa wahusika nchini Tunisia kuhakikisha kuwa watu hawakamatwi kiholela na kwa wale wote wanaokamatwa wanaheshimiwa kwa haki zao zote kuheshimiwa Aidha amesema kuwa  watawala nchini Tunisia lazima wahahakikishe kuwa  yeyote yule anaetimiza haki yake ya kujieleza  pamoja na uhuru wa kukusanyika  hazuiliwi kufanya hivyo. Pia amesem akuwa  wakati huu ikiwa inasubiriwa  kuadhimisha  mapinduzi ya mwaka 2011 yaani januari 14, ni jambo la umuhimu sana  kuwa waandamanaji wanafanya hivyo kwa njia za amani.

Bwana Colville anatoa mwito.

(SAUTI YA RUPERT COLVILLE)

“ Tunaelewa kumetokea wizi wa ngawira, uharibifu wa mali pamoja na ghasia miwemo uharibifu wa  vituo vya polisi na maduka. Tunawaombawaandamanaji  kujizuia na kuwa watulivu. Wanaoandamana kwa   amani hawapaswi kulaumiwa  kuhusika na  visa vya ghasia na kuweza kuaadhibiwa.”

Ofisi hiyo ya haki za binadamu pia imetoa wito wa to work together towards resolving, with full respect for human rights, the economic and social problems underpinning the unrest. The UN Human Rights Office in Tunisia will continue to closely monitor the situation.