Usalama wa chakula CAR shakani
Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati machafuko yamesababisha hali tete ya usalama wa chakula na hivyo kuongeza kadhia kwa raia wa nchi hiyo mjini na vijijini.
Watoto wanakumbwa na hatari ya utampiamlo huku afya ya jamii kwa ujumla ikizorota. Ungana na Grace Kaneiya katika makala inayofafanua madhila hayo na juhudi za Umoja wa Mataifa katika kutoa usaidizi.