Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kupunguza maafa ni muhimu kwa ajenda ya maendeleo: Wahlström

Kupunguza maafa ni muhimu kwa ajenda ya maendeleo: Wahlström

Mwakilishi maalum  wa Katibu Mkuu katika kupunguza majanga Margareta Wahlström amesema mkutano wa kupunguza majanga unaoendelea mjini Sendai Japan una lengo la kuandaa mkakati wa pamoja kwa ajili ya kupunguza maafa hatari  baada ya mwaka 2015.

Katika mahojiano  na redio ya Umoja wa Mataifa kiongozi huyo amesema mkutano huo pia unakusudia kupitia mkataba uliosainiwa  miaka 10 iliyopita mjini Hyogo Japan, kwa lengo la maandalizi bora kupunguza athari za maafa.

Aidha, Wahlström amesema  kuwa nchi lazima zitathmini mipango ya maendeleo endelevu  na jinsi ya kukabiliana mabadiliko ya tabia nchi.

Amesema mwishoni mwa mkutano huo lazima kuwe na makubaliano ya pamoja ya kupunguza hatari ya maafa kwa zama za baada ya mwaka 2015 ambayo yanaenda sambasamba na ajenda ya maendeleo ya makabiliano ya mabadiliko ya tabia nchi.