Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tanzania yajivunia kutimiza malengo 4 kati ya 8 ya milenia:Kikwete

Tanzania yajivunia kutimiza malengo 4 kati ya 8 ya milenia:Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amesema Tanzania inajivunia kutanabaisha kwamba malengo manne kati ya manane ya maendeleo ya Milenia yametimizwa. Akizungumza katika mjadala mkuu wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa Ijumaa jioni amesema…

(SAUTI YA KIWETE)

Ameongeza kuwa kuna haja ya kuendeleza utekelezaji wa kutimiza malengo hayo hata baada ya mwaka 2015. Akimulika migogoro barani Afrika amesemaTanzaniainasikitishwa na maisha ya watu yanayoendelea kutoweka kila uchao katika mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia yaCongo.

(SAUTI YA KIKWETE)

Kwa upande waSyriaameupongeza Umoja wa mataifa na hasa baraza la usalama kwa jinsi ilivyoshugulikia na kuendelea kulitafutia ufumbuzi suala laSyriakwani nchi yake inaamini uuvamizi wa kijeshi ni suluhu ya mwisho kabisa

(SAUTI YA KIKWETE)