Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa WFP ziarani Malawi

Mkuu wa WFP ziarani Malawi

Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, Ertharin Cousin, amewasili nchini Malawi kwa ziara ya siku mbili. Taarifa zaidi na Joshua Mmali.

(Taarifa ya Joshua)

Ziara hiyo inafuatia mafuriko yaliyotokea Malawi mwezi Januari ambapo zaidi ya watu milioni moja wameathirika na wengine 600,000 wakihitaji misaada ya chakula.

Akiwa Malawi, Bi Cousin atatembelea mradi wa mlo wa mashuleni katika wilaya ya Mangoshi. Aidha atakutana na wakulima wadogo wadogo wanaotoa chakula kwa ajili ya mradi huo na ataenda pia katika jamii iliyoathirika na mafuriko na ambayo bado inapokea misaada ya WFP.

Halikadhalika, Mkuu wa WFP atakutana na viongozi, wafadhili na washiriki wa WFP nchini humo.