Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Kenya na mikakati ya kukabiliana na COVID-19 wakati idadi ya wagonjwa ikiongezeka
Katika makala ya wiki hii tunakwenda Nairobi nchini Kenya, mwandishi wetu Jason Nyakundi anamulika harakati za kukabiliana na virusi vya Corona au COVID-19 na changamoto zitokanazo na hatua za kudhibiti kusambaa kwa virusi hivyo
COVID-19 umeathiri pia wachoraji vibonzo lakini mtandao unasaidia
Ripoti ya hivi karibuni ilizotolewa na shirika la kazi duniani ILO ambayo inakubaliana na taarifa za shirika la fedha duniani IMF, inaonesha kuwa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19, sekta ya ajira itaathirika kwa kiasi kikubwa na hivyo kuathiri uchumi wa dunia.
Hata sisi wachora vibonzo, COVID-19 imeathiri kazi zetu-Nathan Mpangala
Ripoti ya hivi karibuni ilizotolewa na shirika la kazi duniani ILO ambayo inakubaliana na taarifa za shirika la fedha duniani IMF, inaonesha kuwa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19, sekta ya ajira itaathirika kwa kiasi kikubwa na hivyo kuathiri uchumi wa dunia.
Ombi la dola milioni 267.5 litasaidia katika kukabiliana na COVID-19 Kenya
Serikali ya Kenya, Umoja wa Mataifa na wadau wake wa masuala ya kibinadamu wametoa ombi la dharura la dola milioni 267.5 kwa ajili ya kukabiliana na mahitaji ya sasa na ya dharura kwa zaidi ya watu milioni 10. Taarifa kamili na Jason Nyakundi
(Taarifa ya Jason)
Ombi hilo liliotolewa jijini Nairobi, Kenya linalenga kuchagiza ufadhili wa dharura kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mashirika ya kiraia katika kusaidia serikali kukabiliana na mlipuko wa wa ugonjwa wa virusi vya corona au COVID-19.
UN na wadau watoa ombi la dola milioni 267.5 kusaidia Kenya kukabiliana na COVID-19
Serikali ya Kenya, Umoja wa Mataifa na wadau wake wa masuala ya kibinadamu wametoa ombi la dharura la dola milioni 267.5 kwa ajili ya kukabiliana na mahitaji ya sasa na ya dharura kwa zaidi ya watu milioni 10.