Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hata sisi wachora vibonzo, COVID-19 imeathiri kazi zetu-Nathan Mpangala

Nathan Mpangala mchoraji maarufu wa vibonzo wa nchini Tanzania.
UN Tanzania/ Stella Vuzo
Nathan Mpangala mchoraji maarufu wa vibonzo wa nchini Tanzania.

Hata sisi wachora vibonzo, COVID-19 imeathiri kazi zetu-Nathan Mpangala

Afya

Ripoti ya hivi karibuni ilizotolewa na shirika la kazi duniani ILO ambayo inakubaliana na taarifa za shirika la fedha duniani IMF, inaonesha kuwa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19, sekta ya ajira itaathirika kwa kiasi kikubwa na hivyo kuathiri uchumi wa dunia.

Nathan Mpangala ni mchoraji maarufu wa vibonzo wa nchini Tanzania ambaye anasema tayari kwa namna fulani ameanza kuona athari za mlipuko wa virusi vya corona katika kazi zake, "Mimi ni mmoja wa waathirika kwa sababu nimebadilisha ule utendaji kazi wa kila siku, ni kweli kwamba sisi wachoraji wengi tunakuwa na ofisi za kutekeleza kazi zetu au ni waajiriwa. Mimi nafanya kazi na vyombo vya habari na wakati mwingine nalazimika kwenda kwenye vyomba vya habari lakini kwa kuwepo virusi vya corona sasa kwenda ofisini ni pale tu kunapo ulazima mkubwa."

Bwana Mpangala anasema hivi sasa kwa kuwa anatekeleza agizo la kutokukutana na watu wengi ili kujikinga na ugonjwa, analazimika kutumia mitandao ya kijamii ili kupata mawazo ya kazi zake, "ninategemea mandao kuangalia na wengine kwa mfano wachoraji kutoka nje wanafanya nini kwa mfano kuhusu corona alafu kutoka pale napata mawazo ya kuendeleza kazi zangua."