Ushushaji misaada kutoka angani Gaza ni tone tu baharini - Sigrid Kaag
Mratibu Mwandamizi wa masuala ya Kibinadamu na Ujenzi wa Gaza, Sigrid Kaag leo Machi 7 jioni ya saa za New York, Marekani amewadokeza wanahabari baadhi ya mambo aliyoyawasilisha leo katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililofanya mashauriano ya faragha kuhusu hali ya Gaza.