Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanawake katika kijiji cha Doi DR Congo
UN Photo/Martine Perret

Wanawake na wasichana ni ufunguo wa mustakbali wa DRC: WFP

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yupo ziarani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambapo katika kuelekea siku ya wanawake duniani itakayoadhimishwa Ijumaa Machi 8 wiki hii ametembelea vikundi vya wanawake wajasiriamali wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kuwaingizia kipato . 

Pwani ya Mogadishu, nchini Somalia
UNODC/Jeremy Douglas

Viongozi wa OCHA na FAO kuadhimisha siku ya wanawake duniani nchini Somalia

Ziara ya Naibu Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA Bi. Joyce Msuya na Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO Beth Bechdol nchini Somalia imewaonesha namna takriban watu milioni 7 walivyo na uhitaji wa msaada wa haraka wa kuokoa maisha kutokana na kuathirika na njaa, vita na mabadiliko ya tabianchi.

Timu ya wafanyakazi wa shirika la UNRWA wakiendelea kugawa msaada wa unga Kusini mwa Gaza ingawa msaada huo hautoshelezi kukidhi mahitaji
© UNRWA

Njaa yaendelea kukatili maisha ya watoto Gaza: UN

Zikiwa zimesalia siku chache tu kabla ya kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani na kukiwa hakuna makubaliano ya kusitisha mapigano yanayotarajiwa kwa Gaza, wahudumu wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa leo wameelezea wasiwasi wao mkubwa kwamba kuna idadi kubwa inayoongezeka ya watoto wanaokufa kwa njaa.

Kijana mkimbizi wa Syria nchini Jordan anasoma katika kituo kinachofadhiliwa na UNICEF.
© UNICEF/Christopher Herwig

Tunawaangusha wakimbizi wa Syria na jamii zinazowahifadhi yaonya UNHCR/UNDP

Wakati mzozo wa Syria ukiingia katika mwaka wake wa 14, eneo hilo linakabiliwa na hali ya kutisha ambapo mahitaji ya wakimbizi wa Syria na jamii zinazowahifadhi yanaongezeka huku ufadhili wa kuwasaidia wakimbizi hao ukiendelea kupungua umeonya leo Umoja wa Mataifa na kuongeza kuwa haya yanajiri katika wakati mgumu sana na tete katika eneo hilo.