Janga Gaza: Kiwango gani kifikie ndio iwe imetosha? Ahoji Rais wa UNGA78 akiwa Uganda
Dunia ikikabiliwa na changamoto kubwa na lukuki zinazohitaji ubunifu, maridhiano na majawabu fanisi, kinachofanyika ni kinyume chake kwani mgawanyiko unaongezeka na fursa za kupata majawabu zinazidi kuwa finyu, amesema Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Balozi Dennis Francis.