Mkuu wa IAEA asema shirika limefikia "Njia Panda" kikazi, lahitaji misaada maridhawa kuendesha shughuli zake
Ijumatatu, tarehe 29 Septemba (08) Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) lilianzisha rasmi mkutano wa mwaka, uliohudhuriwa na wawakilishi kutoka Mataifa Wanachama 145. Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Mohamed ElBaradei alisema kwenye hotuba yake ya ufunguzi, na ninamnukuu hapa, “hali ya kazi katika IAEA hairidhishi na sio nzuri.”