WFP yalalama kuporomoka kwa misaada ya chakula duniani
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limewasilisha ripoti mpya yenye mada isemayo: "Mtiririko wa Misaada ya Chakula Kimataifa", ambayo inatathminia huduma za ugawaji wa chakula ulimwenguni. Ripoti ilibainisha posho la chakula linalogaiwa umma wa kimataifa liliteremka sana katika 2007, kwa kiwango cha asilimia 15. Kiwanago hiki ni cha chini kabisa kushuhudiwa kimataifa tangu mwaka 1961.