Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makundi yanayohasimiana Usomali kuridhia mwafaka wa amani

Makundi yanayohasimiana Usomali kuridhia mwafaka wa amani

Makundi yanayohusika na mgogoro wa Usomali Ijumatatu yalibadili nia na kuamua kutia sahihi maafikiano ya amani kwa lengo la kukomesha uhasama kati yao. Maafikiano haya yalitiwa sahihi nchini Djibouti baina ya wajumbe wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho la Usomali (TFG) pamoja na wawakilishi wa upinzani wa Jumuiya ya Ukombozi wa Pili wa Usomali.