Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ripoti mpya kumurika mafanikio/pingamizi katika kupiga vita UKIMWI

Ripoti iliotayarishwa bia na Jumuiya ya Mashirika ya UM dhidi ya UKIMWI (UN-AIDS), pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) imethibitisha mnamo mwisho wa 2007, watu milioni 3 wenye virusi vya UKIMWI, katika nchi zinazoendelea za pato la chini na kati kiuchumi, walifanikiwa kupatiwa zile dawa maalumu za kurefusha maisha, dawa zijulikanao kwa umaarufu kama dawa za ARV.

IAEA itapeleka wataalamu Syria kuchunguza madai ya shughuli za siri

Mohamed ElBaradei, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Udhibiti wa Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) Ijumatatu aliwasilisha ripoti yake mbele ya wajumbe 35 wa Bodi la Utendaji, linalokutana hivi sasa mjini Vienna kuhusu kazi za taasisi. Aliarifu kwamba mwezi Aprili IAEA ilipokea taarifa zilizodai "kituo cha umeme” nchini Syria, kilchoipigwa makombora na ndege za Israel mwezi Septemba 2007, kilikuwa kikiendeleza shughuli zisio halali. Kwa sababu hizo, alisema ElBaradei, kuanzia Juni 22 hadi 24, IAEA itapeleka tume maalumu ya wataalamu kuchunguza kama kuna uwkeli kutokana na tetesi za Marekani na Israel zilizodai Syria ilishiriki kwenye huduma za siri za kinyuklia.