Ripoti mpya kumurika mafanikio/pingamizi katika kupiga vita UKIMWI
Ripoti iliotayarishwa bia na Jumuiya ya Mashirika ya UM dhidi ya UKIMWI (UN-AIDS), pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) imethibitisha mnamo mwisho wa 2007, watu milioni 3 wenye virusi vya UKIMWI, katika nchi zinazoendelea za pato la chini na kati kiuchumi, walifanikiwa kupatiwa zile dawa maalumu za kurefusha maisha, dawa zijulikanao kwa umaarufu kama dawa za ARV.