Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Moja ya vyumba katika maktaba binafsi ya Little Voice Deep Within  mtaani Kariobangi South, Kenya.
Thelma Mwadzaya

Maktaba ya Little Voice Deep Within inavyosaidia watoto katika maeneo duni Kenya

Siku ya walimu duniani huadhimishwa tarehe 5 Oktoba kila mwaka.Mada kuu kwa mwaka huu ni walimu tunaohitaji kwa elimu tunayoitaka. Kenya imepiga hatua kwenye sekta ya elimu kwa kuzindua mfumo unaojikita katika kukuza vipaji na uwezo wa mwanafunzi, CBC,ila uhaba wa walimu ni kikwazo cha utekelezaji. Baadhi ya walimu wa kujitegeme wamechukua hatua mikononi mwao na kuanzisha maktaba za binafsi ili kuwapa watoto nafasi ya kusoma nje ya mazingira ya shule.

Sauti
6'19"
Wanaume wakipakua magunia ya vitunguu kutoka kwa lori huko Bamako, Mali, nchi inayoendelea isiyo na bandari. Ukosefu wao wa ufikiaji wa moja kwa moja kwa viungo muhimu vya biashara mara nyingi husababisha nchi zisizo na bandari kulipa gharama kubwa za us…
World Bank/Dominic Chavez

UNCTAD yasema uchumi wa dunia uko njiapanda

Kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa UNCTAD, imezindua leo ripoti yake kuu ya Biashara na Maendeleo ya mwaka 2023 ambayo inachunguza kuimarika kwa uchumi wa dunia na kutoa utabiri wa kinachotarajiwa. Ripoti inaeleza hatua za kisera zinazopaswa kuchukuliwa ili kulinda uchumi wa dunia kutokana na matatizo ya kimfumo ya siku zijazo.

Sauti
2'58"