Mkimbizi kutoka Sudan: Sikuwa nataka kurejea nchini mwangu Sudan Kusini
Wakati maelfu ya wananchi wakikimbia machafuko nchini Sudan mashirika ya Umoja wa Mataifa nayo yana haha huku na kule kuhakikisha wanatoa usaidizi kwa wakimbizi hao.
Wakati maelfu ya wananchi wakikimbia machafuko nchini Sudan mashirika ya Umoja wa Mataifa nayo yana haha huku na kule kuhakikisha wanatoa usaidizi kwa wakimbizi hao.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amezungumza na waandishi wa Habari hapa kwenye makao makuu ya Umoja huo muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake na amani na usalama.
Akili mnemba imebadili fani ya sanaa na utamaduni kwa njia ambazo ha ikutarajiwa. Hata hivyo mabadiliko hayo ni ya muda mrefu.
Baada ya kimbunga Idai kupiga Msumbiji mwezi Machi mwaka 2019, maisha ya watoto ‘yalitumbukia nyongo’ kwani hawakuwa ten ana matumaini ya mustakabali wao, halikadhalika wazazi wao. Mapaa ya shule yalienguliwa, hospitali zilitwama, halikadhalika makazi yao.
Siku ya walimu duniani huadhimishwa tarehe 5 Oktoba kila mwaka.Mada kuu kwa mwaka huu ni walimu tunaohitaji kwa elimu tunayoitaka. Kenya imepiga hatua kwenye sekta ya elimu kwa kuzindua mfumo unaojikita katika kukuza vipaji na uwezo wa mwanafunzi, CBC,ila uhaba wa walimu ni kikwazo cha utekelezaji. Baadhi ya walimu wa kujitegeme wamechukua hatua mikononi mwao na kuanzisha maktaba za binafsi ili kuwapa watoto nafasi ya kusoma nje ya mazingira ya shule.
Kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa UNCTAD, imezindua leo ripoti yake kuu ya Biashara na Maendeleo ya mwaka 2023 ambayo inachunguza kuimarika kwa uchumi wa dunia na kutoa utabiri wa kinachotarajiwa. Ripoti inaeleza hatua za kisera zinazopaswa kuchukuliwa ili kulinda uchumi wa dunia kutokana na matatizo ya kimfumo ya siku zijazo.
“Safari ilikuwa ngumu sana, tulikuwa barabarani kwa saa kati ya 26 hadi 29.” Ni simulizi ya mmoja wa wakimbizi zaidi ya 100,000 wanaomiminika Armenia wakitokea eneo la Karabakh linalozozaniwa kati ya Armenia na Azerbaijan.