Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Ripoti ya UNESCO kuhusu tasnia ya filamu barani Afrika inataka kuimarisha tasnia hiyo kwa kuwa inaweza kufungua fursa za ajira na kipato.
Picha na Jeremy Bishop on Unsplash

Waandaji filamu Kenya, Tanzania na Uganda ni miongoni mwa washindi wa awali wa shindano la UNESCO na Netflix

Waandaaji watano wa filamu kutoka Afrika Mashariki ni miongoni mwa waaandaji filamu 21 kutoka barani Afrika ambao wamepita katika mchujo wa awali wa shindano la shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO pamoja na kampuni ya kutengeneza na kusambaza filamu, Netflix la kutengeneza filamu za hadithi za kiafrika.

Tangu Novemba 2020, mzozo kaskazini mwa Ethiopia umesababisha mamilioni ya watu kuhitaji usaidizi na ulinzi wa dharura.
© UNICEF/Christine Nesbitt

Kuna wakati nalala bila kula – Mjamzito nchini Ethiopia

Tathmini mpya ya uhakika wa upatikana wa chakula iliyotolewa mwishoni mwa mwezi Januari 2022 na Shirika la Umoja wa Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula la Umoja wa Mataifa WFP, inaonesha takriban asilimia 40 ya wakazi wa Tigray Ethiopia wanakabiliwa na ukosefu mkubwa wa chakula ikiwa ni miezi 15 ya migogoro kaskazini mwa Ethiopia.

Audio Duration
2'30"
Barakoa iliyopatikana wakati wa kusafisha ufukwe wa Hampton, New Hampshire, USA.
Unsplash/Brian Yurasits

Taka zilizotokana na kudhibiti COVID-19 zafichua hitaji la dharura kuboresha mifumo ya udhibiti wa taka 

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO limetoa ripoti mpya inayoonesha kuwa mifumo ya usimamizi wa taka za afya duniani kote hivi sasa imezidiwa uwezo kutokana na maelfu ya tani za taka zinazotokana na vifaa vilivyotengenezwa kwa ajili ya kukabiliana na janga la COVID-19 na hivyo kutishia afya ya binadamu na mazingira na wakati huo huo kufichua hitaji kubwa la kuboresha udhibiti wa taka zinazozalishwa kutokana na huduma ya tiba.  

Sauti
2'44"