Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

Dr.Alinda Mashiku

Penye nia pana njia kama nimefika NASA nawe utaweza: Mhandisi Dkt.Alinda Mashiku 

Mwanamke Mtanzania angara kituo cha safari za anga cha Marekani NASA  tawi la Goddard mjini Maryland lililojikita na ufuatiliaji wa safari za satellite. Dkt. Alinda Mashiku ambaye amekuwa NASA kwa miaka minane sasa anasema ilimchukua miaka 12 hadi kuajiriwa NASA kama mhandisi na sasa pia ni meneja wa kitengo cha kuhakikisha satellite zonazokwenda angani hazigongani. Je anahisi vipi kuwa miongoni mwa wanawake wachache wahandisi NASA na safari yake ilianza vipi? Kufahamu yote hayo na mengine mengi ungana na Flora Nducha wa UN News Kiswahili aliyeketi na kuzungumza naye katika makala hii  

Audio Duration
13'39"
Oscar Ikinya

Miaka 23 baada ya tukio la ugaidi Kenya bado athari zipo-Oscar Ikinya

Wakati dunia imeadhimisha siku ya kimataifa ya kumbukumbu na kuwaenzi waathirika wa ugaidi Agosti 21 Umoja wa Mataifa unasisitiza umuhimu wa kuendelea kushikamana na waathirika kwani Maisha yao yanabadilika kwa kiasi kikubwa kufuatia matukio waliyoyapitia, Hali ni kama hiyo kwa mgeni wetu wa leo manusura wa shambulio la kigaidi la Kenya la mwaka 1998. Amezungumza na Grace Kaneiya akiwa Nairobi Kenya kwa njia ya mtandao. Katika mazungumzo safari imeanzia miaka 23 iliyopita wakati wa tukio hadi sasa. Karibu.

Sauti
28'51"