Shughuli zake si ofisini tu bali pia zinahusisha kwenda mashinani. Naibu Katibu Mkuu Amina J. Mohammed na Malala Yousafzai, Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel na Mjumbe wa Amani wa Umoja wa Mataifa, wanakutana na wanafunzi katika Kituo cha Mafunzo cha Lafiya Sariri, katika jimbo la Borno, Kaskazini-mashariki mwa Nigeria.
Kuwa kinara na mwenyekiti wa maendeleo endelevu haimaanishi hatekelezi majukumu mengine ya pamoja ya Umoja wa Mataifa. Katika Picha ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres (Katikati) akiwasilisha Tamko jipya la Kisera kuhusu Ajenda Mpya ya Amani, ambayo inaelezea maono yake ya juhudi za kimataifa za amani na usalama, kwa kuzingatia sheria za kimataifa.
Pembeni yake (Kulia) ni Naibu Katibu Mkuu Amina J Mohammed pamoja na wengine wote kwenye picha ni wasaidizi wa Katibu Mkuu katika masuala mbalimbali.
Naibu Katibu Mkuu Amina Mohammed (katikati) akikutana na Noor bint Ali AlKhulaif, Waziri wa Maendeleo Endelevu wa Bahrain (kulia), na Amna bint Ahmed Al-Rumaihi, Waziri wa Nyumba na Mipango Miji wa Bahrain.
Lengo namba 11 la SDGs linahimiza kila nchi kuhakikisha majiji pamoja na makazi ya watu wote kuwa salama, imara na endelevu.
Naibu Katibu Mkuu Amina J Mohammed akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP Cindy McCain walisafiri mpaka kwenye mpaka wa nchi za Chad na Sudan, ambako idadi ya wakimbizi wa Sudan wanaingia nchini Chad wakikimbia ghasia inayoendeleea kuongezeka sana. Wakiwa mpakani walisikia simulizi nyingi za kusikitisha za wananchi wanaoingia Chad kusaka hifadhi. UN inafanya kazi kwa bidii na washirika wake ili kutoa usaidizi wa kuokoa maisha.
Akiwa ziarani katika ukanda wa mashariki nchini Chad, Naibu Katibu Mkuu AminaJMohammed alitembelea eneo la michezo ya watoto katika kambi ya wakimbizi ya Farchana, ambapo
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF linatoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto wakimbizi na kuwasaidia kuondokana na kiwewe baada ya kushuhudia machafuko nchini mwao Sudan.