Wanawake wamesalia nguzo kuu hata katikati ya janga la COVID-19
Hii leo ikiwa ni siku ya wanawake duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la COVID-19 limefuta maendeleo ya miongo kuelekea usawa wa jinsia huku wanawake wakikumbwa zaidi na machungu, bado kundi hilo limesalia kuwa mstari wa mbele kwenye hatua dhidi ya janga la Corona.