Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Kaskazini mwa Gaza iko kwenye magofu baada ya miezi kadhaa ya mashambulizi ya mabomu.
© WFP/Ali Jadallah

Wananchi wa Gaza wako katika jakamoyo wakisubiri taarifa kuhusu wito wa kusitisha mapigano: UN

Wakati kukiwa na ongezeko la wito wa kimataifa kwa Israel kujizuia na mashambulizi zaidi Gaza na ripoti za leo za mashambulizi mengine mabaya zaidi ya usiku kucha, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamesisitiza kuhusu athari mbaya zinazoendelea za vita hiyo na haja ya kuhakikisha njia za kuaminika za usambazaji wa misaada kwa watu wanaohitaji kwa udi na uvumba zinapatikana. 

Sauti
1'57"
Watu wakiwa wamekusanyika nje ya Hospitali ya Al Shifa Gaza ambako kumepatikana makaburi ya halaiki
WHO

GAZA: Makaburi ya halaiki yaonesha waathirika walikuwa wamefungwa mikono - OHCHR

Ripoti za kutisha zinaendelea kuibuka kuhusu makaburi ya halaiki huko Gaza ambako waathirika wa Kipalestina wameripotiwa kuvuliwa nguo wakiwa wamefungwa mikono, jambo ambalo limezusha wasiwasi juu ya uwezekano wa  kuweko kwa vitendo vya uhalifu wa kivita huku kukiwa na mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR.

Baraza Kuu lilipitisha azimio mwaka 2012 lililoipa Palestina hadhi ya kuwa nchi isiyokuwa mwanachama katika Umoja wa Mataifa. (faili)
UN Photo/Rick Bajornas

Hadhi ya Palestina ndani ya UN yafafanuliwa 

Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.