Ghasia mpya Kasai zinaweza kuchochea wimbi jipya la ukimbizi- UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, leo limeonya kuwa ghasia mpya zinazoibuka katika eneo la Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, zinaweza kuibua wimbi kubwa la ukimbizi iwapo hali ya sasa haitaimarishwa.