Vurugu dhidi ya ofisi za UN DRC: Serikali kuwasaka na kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imesihi utulivu miongoni mwa wananchi baada ya maandamano na uvamizi dhidi ya vituo vya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kwenye miji ya Goma na Butembo jimboni Kivu Kaskazini, tukio ambalo hata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka mamlaka zichunguze na sheria ichukue mkondo wake. Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ana taarifa zaidi.