Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DR Congo

Kambi ya wakimbizi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNOCHA

Mkutano wa kirafiki wakutanisha walinda amani kutoka Tanzania na baadhi ya viongozi mashariki mwa DRC

Kuelekea siku ya kimataifa ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa na katika kuendeleza jukumu la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,  vikosi vya ulinzi wa amani kutoka Tanzania yaani TANZBATT 9 na kikosi cha utayari TANZANIA QRF2 vimefanya kikao cha Urafiki baina yao na uongozi wa raia wa nchi hiyo katika maeneo ya uwajibikaji wa vikosi hivyo.

Sauti
3'17"
Uzinduzi wa mpango wa kusaidia askari wa zamani wa msituni na vijana walio kwenye mazingira hatarishi ili waweze kujipatia kipato. Hapa ni Nyiragongo, jimboni Kivu Kaskazini na mradi unatekelezwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO
MONUSCO/Michael Ali

MONUSCO na COMOA washirikiana kuimarisha usalama Goma, DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kupitia kitengo chake cha kupokonya silaha askari waliojisalimisha, kuvunja makundi na kujumuisha askari hao katika jamii, DDR umepatia shirika la kiraia liitwalo COMOA, takribani dola 50,000 ili kufunga taa 60 za sola kwenye kitongoji cha Karuba kilichoko takribani kilometa 50 kutoka mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, Goma.

 

Sauti
2'38"
Maji safi ya kunywa
World Bank/Arne Hoel

Mradi wa maji wadhibiti kipindupindu DRC 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa ushirikiano na kituo cha kimarekani cha kudhibiti magonjwa, CDC wamesaidia ujenzi wa tenki za maji kwa ajili ya wakazi wa Kiziba mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na hivyo kusaidia kuepusha maambukizi ya magonjwa yatokanayo na matumizi ya  maji machafu. 

Sauti
2'9"