Msako dhidi ya watetezi wa haki Burundi watia hofu UN
Ofisi ya Kamishna wa Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa hii leo imesema ina hofu kubwa juu ya ongezeko la msako dhidi ya watetezi wa haki nchini Burundi kufuatia kuswekwa korokoroni hivi karibuni kwa watetezi watano wa haki za binadamu na kufungwa jele kwa mwandishi wa Habari.