Heko Tanzania kwa kuendelea kuwa kimbilio la waliofurushwa makwao- Grandi
Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi amekuwa na mazungumzo na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili maendeleo katika kuweka mazingira mazuri kwa wakimbizi wa Burundi walioko nchini humo kurejea nyumbani.