Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Vital Bambanze (kulia) mwakilishi wa jamii ya watwa nchini Burundi akiwa kwenye majadiliano na washiriki wengine wakati wa mkutano wa 21 wa jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFII mwezi Aprili 2022 jijini New York, Marekani.
UN/ Flora Nducha

Nuru Burundi kwa haki za jamii ya Watwa

Mkutano wa 21 wa Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFFII likiwa limeingia siku ya tatu kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani, washiriki kutoka Burundi wameieleza Idhaa ya Kiswahili ya  Umoja wa Mataifa juu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha haki za binadamu za jamii ya asili aina ya watwa zinazingatiwa.