Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 imepunguza uchafuzi wa hewa lakini sio mbadala wa hatua za mabadiliko ya tabianchi:WMO
Kushuka kwa kiwango cha gesi chafuzi kunakohusiana na mlipuko wa janga la virusi vya corona au COVID-19 ni Habari njema za muda mfupi kwa mujibu wa mkuu wa shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO.
Ni lazima tuilinde sayari dunia na watu wake-Guterres
Janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 limefanya macho yote ya Dunia kuelekezwa kwenye mtihani huu mkubwa zaidi ambao ulimwengu umekumbana nao tangu Vita vya Pili vya Dunia amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Antonio Guterres katika ujumbe wake maalum wa siku ya kimataifa ya mama sayari Dunia hii leo amesema
22 APRILI 2020
Leo katika jarida la Umoja wa Mataifa Flora Nducha anakuletea
-Umoja wa Mataifa unasema janga la virusi vya Corona au COVID-19 ni kengele ya kuiamsha dunia kuchukua hatua kulinda sayari hiyo na watu wake hasa leo ikiadhimishwa siku ya kimataifa ya mama sayari dunia
- Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na jiji la Nairobi wanachukua hatua kudhibiti kusambaa wa virusi vya corona au COVID-19, kwenye makazi dunia ya Kibera.
Linapokuja suala la wakimbizi na COVID-19 ni bora kukinga kuliko kuponya:UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wadau wake nchini Bangadesh wanachukua kila tahadhari ili kuhakikisha maelfu ya wakimbizi wa Rohingya kwenye moja ya makazi makubwa kabisa ya wakimbizi duniani ya Cox's Bazaar wanalindwa dhidi ya mlipuko wa Corona au COVID-19.
Janga la COVID-19 ni kumbusho la umuhimu wa sayari dunia:Guterres
Janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 limefanya macho yote ya Dunia kuelekezwa kwenye mtihani huu mkubwa zaidi ambao ulimwengu umekumbana nao tangu Vita vya Pili vya Dunia amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa